Katika Mkutano wa Kusikiliza dai lako la Ukimbizi

Usikilizaji wa ombi lako la ukimbizi ndio tukio kuu katika mchakato huu. Jifunze ni nini cha kutarajia siku yako ya kusikilizwa. Elewa nani atakuwepo na majukumu yao ni gani. Kuwa tayari kuhudhuria usikilizaji wa ombi lako kwenye mtandao au ana kwa ana.

Kuhusu Mkutano wa Kusikiliza Wakimbizi

Kusikilizwa kwa dai lako la ukimbizi ndio sehemu muhimu zaidi ya huu mchakato. Wakati wa kusikilizwa kwako, au baada ya kusikilizwa kwako, utagundua kama dai lako la ukimbizi limekubaliwa au limekataliwa.

Mkutano wa kusikilizwa dai lako ni fursa yako ya kusimulia hadithi yako na kueleza ni kwa nini unahitaji ulinzi wa Kanada. Huu mkutano ni wa faragha na ni salama.

Wakati wa mkutano wa kusikiliza ombi lako unaweza kujisikia ni kama uko mahakamani lakini sio hivyo. Wanaofanya maamuzi wanaitwa Wanachama na wamepewa mafunzo maalum ya kuamua madai ya ukimbizi. Mwanachama ataamua dai lako kwa haki.

Mikutano ya kusikiliza wakimbizi kwa kawaida huchukua muda wa masaa 3-4, lakini unaeza kuwa mrefu au mfupi zaidi kulingana na mambo yatakavyokwenda. Mikutano hii mara nyingi hufanywa mtandaoni, ila mengine yanafanyika ana kwa ana katika ofisi ya IRB.

Nani atakuwepo kwenye Mkutano wako wa Ombi la Ukimbizi?

Mikutano ya kusikiliza maombi ya wakimbizi ni ya faragha na hayaruhusu umma kuhudhuria. Ni watu fulani pekee wanaweza kuhudhuria kikao chako cha ombi la mkimbizi:

Mwanachama wa IRB-RPD

Mtoa-uamuzi katika kikao chako anaitwa Mwanachama. Mwanachama wa IRB-RPD anaendesha kesi na anaamua kukubali au kukataa dai lako. Mwanachama anatarajiwa kukuongolesha kwa heshima na uangalifu. Mwanachama atasoma Fomu yako ya BOC na ataangalia ushahidi wako wote kabla na mkutano kuanza. Atakuuliza maswali wakati wa kusikilizwa kwako ili kumsaidia kufanya uamuzi kuhusu dai lako la ukimbizi.

Mwakilishi wa kisheria

Mwakilishi wako wa kisheria anaweza kuwa wakili, mshauri wa uhamiaji, au mwakilishi wa kujitolea. Katika jimbo la Quebec, Mthibitishaji wa umma anaweza kukuwakilisha, na katika jimbo la Ontario, mwanasheria anaweza kukuwakilisha.

Wakati Mwanachama anakuuliza maswali, mwakilishi wako wa kisheria anaweza kukuelezea ni nini anamaanisha. Mwakilishi wako wa kisheria hawezi kukujibia maswali. Lazima uwe tayari kumjibu Mwanachama mwenyewe. Mwakilishi wako wa kisheria atakuwa na nafasi ya kukuuliza maswali, lakini kwa kawaida, lazima asubiri mpaka Mwanachama amalize kukuuliza maswali kwanza.

Mwishoni mwa kusikilizwa kwako, mwakilishi wako wa kisheria anaweza kutoa muhtasari wa dai lako kwa Mwanachama. Hii inaitwa mawasilisho. Mawasilisho yanaweza kufanywa kwa kumuambia Mwanachama kwenye kikao cha kusikilizwa, au yanaweza kuandikwa kwenye barua na mwakilishi wako wa kisheria na kutumwa kwa IRB-RPD baada ya kusikilizwa kwako.

Wakili wa Waziri

Wakili wa Waziri ni mfanyakazi wa CBSA au IRCC. Wakili wa Waziri hahusiki katika madai ya kila mtu ya ukimbizi. Watahusika ikiwa wanataka kupinga dhidi ya dai lako la ukimbizi. Ikiwa Wakili wa Waziri anahusika, ni kwa sababu wana wasiwasi:

  • kuhusu wewe ni nani au kuhusu hati zako,
  • kwamba hujasema ukweli, au
  • kwamba wewe ni mhalifu au wewe ni mwanachama wa shirika la kigaidi.

Utajulishwa kama Wakili wa Waziri atahusika katika madai yako. Kabla ya kusikilizwa, Wakili wa Waziri atakutumia wewe au mwakilishi wako wa kisheria Notisi ya Kuingilia kati. Katika notisi, wanaelezea jinsi watahusika na kwa nini watahusika. Notisi itasema kama watakuja kwenye kusikilizwa kwako au kama watatuma hati tu. Unapaswa kupata notisi angalau siku kumi au zaidi kabla ya kusikilizwa kwako. Isome kwa makini na uwe tayari kuizungumzia. Ikiwa Wakili wa Waziri yuko kwenye kikao chako, kuna uwezekano atakuuliza maswali.

Mkalimani

Jukumu la mkalimani ni kuhakikisha kwamba kila mtu anamuelewe mwengine vizuri. Hata kama unajua Kiingereza au Kifaransa, ni vizuri kuwa na mkalimani ili kuepuka makosa. Wakalimani wa IRB hawatatoa habari zozote kukuhusu au kuhusu dai lako kwa mtu yeyote asiyehusika katika mkutano huo.

IRB-RPD itakupatia mkalimani mtaalamu bila malipo kwako anayejua lugha na lahaja yako. Ikiwa hukusema kuwa unataka mkalimani katika fomu yako ya BOC, bado unaweza kumuitisha. Andika kwa IRB-RPD siku kumi au zaidi kabla ya kusikilizwa kwako ili kuomba upewe mkalimani.

Unaweza kuomba mkalimani wa jinsia mahususi au wa jinsia sawa na wewe ikiwa ungejisikia vizuri zaidi na hili. Kwa mfano, kama dai lako la ukimbizi linatokana na jambo nyeti lililokutokea na utaona ni rahisi kuwa na mkalimani ambaye ni jinsia sawa na wewe, wajulishe IRB-RPD.

Mashahidi

Unaweza kuwa na mashahidi katika kusikilizwa kwako watakao zungumza kuhusu madai yako. Shahidi ni mtu ambaye anaweza kuthibitisha kilichotokea kwako. Mashahidi wanaweza kuwa ndani ya Kanada au katika nchi nyingine. Shahidi pia anaweza kuwa mtu mwenye utaalamu kuhusu masuala yanayohusiana na dai lako la ukimbizi.

Chagua mashahidi wako kwa uangalifu ukitumia usaidizi wa mwakilishi wako wa kisheria. Hakikisha unawatayarisha mashahidi kabla ya kusikilizwa kwako. Wajulishe mashahidi wako kwamba watachosema lazima kiwe cha kweli. Iwapo ungependa kualika mashahidi kwenye kikao chako, wewe au mwakilishi wako wa kisheria, ni lazima muandike kwa IRB-RPD (na pia kwa Wakili wa Waziri ikibidi) siku kumi au zaidi kabla ya kusikilizwa kwako. Wape:

  • Jina la shahidi wako
  • Taarifa fupi ikieleza kwa nini wanazungumza
  • Uhusiano wako na shahidi
  • Unadhani wataongea kwa mda gani

Watazamaji

Unaweza kualika mtazamaji mmoja au zaidi kwenye kikao chako cha mkimbizi kama itakusaidia ujiskie vizuri. Mtazamaji anaweza kuwa rafiki, jamaa, au mtu wa jumuiya yako.

Katika kusikilizwa kwako, Mjumbe atawauliza watazamaji wajitambulishe. Wakati wa kusikilizwa, watazamaji hawaruhusiwi kuzungumza na lazima watulie. Mtazamaji hawawezi pia kuwa shahidi.

Watoto wako wenye umri wa miaka 18 au chini

Ikiwa una watoto walio na umri wa miaka 18 au zaidi, lazima waje kwenye kikao cha kusikilizwa kwa wakimbizi. Watoto walio chini ya umri wa miaka 18 si lazima waende kwenye kikao hicho isipokuwa ikiwa Mwanachama amewaita. Kwa usikilizaji wa mtandaoni, hakikisha kuwa kuna mtu atakaye wangalia watoto wako wadogo kando na mahali ulipo. Unaweza kuwa unazungumzia matukio mabaya. Haya ni mambo ambayo huenda hutaki watoto wako wayasikie. Ikiwezekana, waambie watoto wako waende shuleni au wakae na jamaa au marafiki, au mlipe mtu awaangalie.

Mwakilishi Mteule

IRB-RPD humtaja Mwakilishi Aliyeteuliwa kuwawakilisha watoto wadogo au watu wazima ambao hawawezi kuelewa mchakato wa ukimbizi. Mwakilishi Aliyeteuliwa humsaidia mtu huyo kuelewa kinachotokea na kumsaidia kuunda kesi bora zaidi. Mwakilishi Mteule anaweza kuulizwa maswali wakati wa kusikilizwa. IRB-RPD kwa kawaida huchagua mzazi kama Mwakilishi Aliyeteuliwa ikiwa dai la mtoto limeunganishwa na dai la mzazi wake.

Mikutano ya Mtandaoni na ya Ana kwa ana

Vikao vya kusikiliza madai ya ukimbizi huwa viko aina mbili: vikao vya mtandaoni, na vikao vya ana kwa ana.

Vikao vya Mtandaoni

Vikao vya mtandaoni huwa vinafanywa kwenye mtandao. Mikutano hii hufanyika kwenye kompyuta kutumia Microsoft Teams.

Jitayarishe kwa ajili ya kikao chako cha mtandaoni

Baada ya IRB-RPD kuamua kikao chako kitafanywa siku gani na ni saa ngapi, watakutumia barua ya kukupa taarifa au watamtumia mwakilishi wako wa kisheria. Soma taarifa hii kwa uangalifu kwa sababu itakuelezea ni nini cha kufanya ili uwe uko tayari kuhudhuria kikao chako cha mtandaoni.

Ili kufanya mkutano wako mtandaoni utahitaji:

  • Mtandao wa kuaminika, ulio salama, na wa kasi ya juu
  • Tarakilishi au kompyuta
  • Sehemu ya utulivu na ya siri

Ikiwa una mwakilishi wa kisheria, unaweza kwenda ofisini kwake kuufanya mkutano huu. Jadiliana na mwakilishi wako wa kisheria ili ujue kama hii itawezekana.

Iwapo hutaenda kwa afisi ya mwakilishi wako wa kisheria, hakikisha kuwa una kila kitu unachohitaji ili kuufanya mkutano wako mtandaoni. Ikiwa huna tarakilishi au kompyuta, au huna mtandao, omba usaidizi kutoka kwa IRB-RPD. IRB-RPD wanaweza kukupa tarakilishi na chumba katika ofisi zao ili utumie. Tuma maombi kwa ofisi ya IRB-RPD iliyo katika eneo lako kwa kupiga simu, au kutuma barua, au barua pepe. Lazima uwasiliane nao kwa muda usiopungua wiki mbili kabla ya tarehe ya mkutano wako kufika.

Takriban siku tano kabla ya mkutano wa kusikiliza dai lako, IRB-RPD watamtumia mwakilishi wako wa kisheria tovuti ya kujiunga kwenye mkutano wa kikao chako cha mtandaoni. Mwakilishi wako wa kisheria atakupa tovuti hii. Ikiwa huna mwakilishi wa kisheria, IRB-RPD watakutumia tovuti hiyo kwenye barua ya pepe. Hakikisha kuwa IRB-RPD wana maelezo sahihi ya anwani ya kukutumia barua na barua pepe, pamoja na nambari ya simu unayoitumia.

Katika kikao chako cha mtandaoni

Siku ya kikao cha mtandaoni cha kusikiliza dai lako, utaombwa ujiunge kwenye mkutano dakika 15 kabla ya mkutano huo kuanza. Hii itakupa nafasi ya kuhakikisha kwamba mtandao wako wa intaneti unafanya kazi vyema, utakuwa na muda wa kusalimiana na mfanyakazi wa IRB-RPD, na pia utapata fursa ya kuongea na mkalimani wa IRB ili uhakikishe kuwa mnaelewana kilugha. Mwanachama wa IRB atakapojiunga kwenye mkutano, atazungumza na wewe na kukuuliza uthibitishe kuwa uko peke yako na uko mahali pa faragha. Ikiwa una matatizo yoyote ya kuona au kusikia video wakati wa kikao hiki cha mtandaoni, hakikisha umemjulisha Mwanachama.

Ikiwa hutaki mkutano wako ufanyike mtandaoni

Mikutano ya kusikiliza maombi ya wakimbizi yote huwa yamepangwa yafanyike mtandaoni, lakini kikao chako kinaweza kubadilishwa kikafanywa ana kwa ana.

Lazima ujaze fomu hii na uitume angalau siku kumi kabla ya siku ya kusikilizwa kwa ombi lako. Lazima useme ni kwa nini unataka mkutano wako ufanywe ana kwa ana.

Mikutano ya ana kwa ana

Mikutano ya ana kwa ana huwa inafanyika katika ofisi ya IRB-RPD. Wakati wa mkutano, kila mtu atakuwa yuko kwenye chumba kimoja.

Mkutano wako utafanywa ana kwa ana ikiwa IRB-RPD wataamua hivyo au ikiwa ulituma ombi kikao chako kifanywe ana kwa ana na IRB-RPD wakakubali.

Mikutano ya ana kwa ana hufanyika katika ofisi za IRB-RPD. Baada ya IRB-RPD kuchagua tarehe na saa ya mkutano wako, watakutumia wewe au mwakilishi wako wa kisheria Taarifa ya Kuhudhuria mkutano. Taarifa ya Kuhudhuria mkutano itakupa anwani ambapo mkutano huo utafanyika. Soma taarifa hii kwa uangalifu kwa sababu itakuelezea ni nini cha kufanya.

Katika mkutano wako wa ana kwa ana

Siku ya mkutano wako wa ana kwa ana, hakikisha umewasili angalau dakika 15-30 kabla ya mkutano wako kuanza. Hii itakupa muda wa kukitambua chumba ambacho mkutano utafanyika. Ikiwa una watu waliokuja kukuangalia au una mashahidi wowote, wao pia wanapaswa wafike angalau dakika 15 kabla ya mkutano kuanza. Unaweza kuulizwa usubiri katika chumba cha wageni hadi chumba cha mkutano kiwe tayari. Kabla ya mkutano wako kuanza, fanya mazungumzo na mkalimani ili uhakikishe kuwa mnaelewana lugha.

Siku ya kusikilizwa kwa kesi yako

Kusikizwa kwako kwa kesi utakuwa wa muda gani?

Usikilizaji wa kesi kwa kawaida huchukua nusu siku na mapumziko mafupi katikati ya usikilizaji. Baadhi ya masikilizano ni mafupi, na mengine ni marefu. Ikiwa dai lako linasikilizwa na wanafamilia wengine, au ikiwa kuna masuala mengi ya kujadiliwa, linaweza kudumu siku nzima.

Unaweza kuomba mapumziko wakati wowote wakati wa kusikilizwa kwako ikiwa unahitaji.

Unapaswa kufika lini?

Ni muhimu kufika mapema kwenye usikilizaji wako. Ikiwa usikilizaji wako ni wa mtandaoni unapaswa kuingia kwenye mkutano wa Microsoft Teams mtandaoni dakika 15 kabla ya kuanza kwa usikilizaji wako. Ikiwa usikilizaji wako ni wa kibinafsi unapaswa kufika dakika 15-30 kabla ya kusikilizwa kwako ili kuhakikisha kuwa unaweza kupata chumba cha kusikilizwa.

Je, nini kitatokea kwa kusikilizwa kwako?

1. Utangulizi:

Mwanachama atamtambulisha kila mtu katika chumba na kukueleza mchakato wa kusikilizwa. Utaulizwa kuinua mkono wako wa kulia na kuahidi kusema ukweli.

2. Uthibitisho wa hati:

Mwanachama anaangalia hati zote ambazo zimetumwa kama ushahidi katika dai lako la ukimbizi. Wanahakikisha kila mtu ana nakala ya hati zote na wanapeana kila hati nambari. Mwanachama pia anaweza kuangalia hati zozote asilia ambazo utaleta kwenye kikao.

3. Kuhoji:

Mwanachama atakuuliza maswali. Maswali yanaweza kuwa kuhusu historia yako, hati zako, na masuala ya kisheria ambayo ni muhimu kwa dai lako la ukimbizi. Baada ya Mjumbe kukuuliza maswali, wakili wa Waziri (kama yupo) anaweza kukuuliza maswali. Mwakilishi wako wa kisheria pia anaweza kukuuliza maswali.

4. Mashahidi:

Ikiwa una mashahidi, watazungumza ijayo. Mashahidi wataweza tu kujiunga na usikilizaji wako wakati wao wa kuzungumza nao utakapowadia.

5. Maoni:

Mwishoni mwa kusikilizwa kwako, Mwanachama atampa wakili wako au wewe fursa ya kueleza kwa maneno yako mwenyewe kwa nini unafikiri ushahidi unaonyesha kwamba unakidhi ufafanuzi wa “Mkimbizi wa Mkutano Mkuu” au “Mtu Anayehitaji Ulinzi.” Hii inaitwa mawasilisho. Ikiwa una mwakilishi wa kisheria wanaweza kukubaliana na Mwanachama kutuma mawasilisho haya kwa maandishi baada ya kusikilizwa. Wakili wa Waziri (kama yupo) anatoa maoni yao ya kudumu.

6. Uamuzi:

Mwishoni mwa kusikilizwa, Mwanachama anaweza kukuambia uamuzi wake wa kukubali au kukataa dai lako au anaweza kusema atakutumia uamuzi wake kwa barua. Katika visa vyote viwili, utapokea “Notisi ya Uamuzi” katika barua.

Je, unapaswa kuleta nini kwenye usikilizaji wako?

Katika kusikilizwa kwako unapaswa kuhakikisha kuwa unayo:

  • Fomu ya BOC
  • Simulizi
  • Fomu za uhamiaji
  • Ushahidi
  • barua ya Notisi ya Kutokea

Mwanachama mara nyingi atakuambia usisome kutoka kwa hati zako wakati wa kujibu maswali. Lakini ni muhimu kuwa na hati zako kwako kwa sababu Mwanachama anaweza kukuuliza uangalie sehemu au kurasa maalum katika hati zako.

Je,masikizo ni ya kibinafsi?

Masikizo yote ya wakimbizi ni za siri. Hii ina maana kwamba watu wote wanaoshiriki katika kusikilizwa kwako, akiwemo mkalimani, hawaruhusiwi kushiriki habari kuhusu dai lako na mtu mwingine yeyote.

Unapaswa kufanya nini ikiwa huelewi swali?

Mwanachama akikuuliza swali ambalo huelewi, usijaribu kulijibu. Mwambie Mjumbe huelewi na uwaambie waseme kwa njia tofauti. Usiwahi kutoa jibu. Ikiwa hujui kitu, au huna uhakika, sema hivyo.

Unapaswa kufanya nini ikiwa mkalimani amefanya makosa?

Kazi ya mkalimani ni kutafsiri hasa au kwa karibu iwezekanavyo. Hawapaswi kuongeza chochote au kuacha chochote nje. Ikiwa unafikiri mkalimani anaweza kuwa amefanya makosa au huelewi jambo ambalo limesemwa wakati wa kusikilizwa, ni muhimu sana kumwambia Mjumbe.

Umwiteje Mbunge?

Unaweza kumwita Mwanachama “Bwana” au “Madam”

Je, masikizo imerekodiwa?

Masikizo yote inarekodiwa. Ukipata uamuzi hasi unaweza kuomba nakala ya rekodi. Unaweza kutumia rekodi ili kuonyesha kile kilichosemwa kwenye masikizo ukiamua kukata rufaa.

Unapaswa kufanya nini ikiwa unahisi kukasirika au kuanza kulia?

Usijali, ni sawa kuhisi kufadhaika au kulia wakati wa masikizo yako ya ukimbizi. Ikiwa unapoanza kujisikia hasira wakati wowote wakati wa kusikilizwa, unaweza kuchukua hatua za kujituliza. Kwa mfano:

  • chukua pumzi 3 au 4
  • omba maji
  • omba mapumziko mafupi